Ndoto kuhusu sherehe ya harusi 

Kama ukiota kwamba unaoa ama unaolewa, hii inaweza kuashiria bahati mbaya, hasa kwa wanaume. Inaweza kumaanisha kwamba kutatokea ajali au kifo maishani mwako hivi karibuni. Kama mmoja wa watu waliopo kwenye ndoto yako anaumwa ama ana ulemavu, ndoto hii inaweza kuashiria kwamba utaingia kwenye ndoa isiyo na furaha. Muda pekee ambao ndoto hii huashiria jambo jema ni pale mwanamke anapoota kwamba ameolewa na mzee. 

Sherehe za harusi katika ndoto mara nyingi hutafsiriwa na watu kumaanisha ujio wa msiba. Kama una mgonjwa nyumbani mwako, na kisha mmoja wa wanafamilia yako akaota ndoto inayohusu sherehe ya harusi, basi kuna wanaoamini kwamba ndoto hiyo huashiria kwamba mgonjwa huyo atapoteza maisha.

Leave a Reply